JOGOO LIMEWIKA

Sunday, October 14, 2012

TUKIWA TUNAAMINI KABISA KUA ELIMU NI UFUNGUO WA MAISHA YA WANADAMU BASI IPO HAJA YA KUSHAJIISHA KWA NAMNA TAFAUTI KUKUZA NGUVU YA MUAMKO WA KIELIMU VIJIJINI




 
TATIZO LA UHABA WA MADAWATI NA MAKTABA


kunatabia ya wanafunzi kuhamisha madawati kila muda kutokana na uhaba kutoka chumba kimoja kwenda chumba chengine hii hali inakwaza maendeleo ya masomo kwa kizazi kipya hichi, miongoni mwao ni viongozi mbali mbali na maafisa wa taasisi mbali mbali za Taifa la kesho, ili kua na taifa imara lazima tutupie elimu macho mawili ya huruma kwa vijana hawa kabla hawajakata tamaa.

TUNAHITAJI KUSAIDIA UMALIZAJI WA MADARASA YALIOJENGWA NA NGUVU ZA WAZAZI NA NA WANAFUNZI NA KUISHIA HAPA KAMA INAVOONEKANA

Saturday, October 13, 2012

SAIDIA WANAFUNZI UOKOE NA KUBORESHA TAIFA LA KESHO

KIZAZI HICHI NDIO TAIFA LA KESHO
USHIRIKIANO WA KUWASAIDIA WANAFUNZI VIJIJINI NI MUHIMU SANA ILI NAO KUWEZA KUINGIA KATIKA USHINDANI WA KIELIMU POPOTE BILA KUJALI WAPI WANATOKA AU WAPI KASOMA, IDADI YA WAKAAZI WA VIJIJINI WANANYIMWA MAMBO MENGI SANA YA KIMSAADA WAKIELIMU,HIVYO BASI IPO HAJA NAWAO WAKAWAEZESHWA KUINGIA KATIKA UTANDAWAZI NA KUPATA HUDUMA ZOTE ZAKISHULE KAMA VILE MAKTABA,MAABARA NA VITENDEA KAZI KAMA KOMPUTA NA MADAWATI.

RASILIMALI ZA WATU WA VIJIJINI ZIFAIDISHE WANA VIJIJI WENYEWE

VIJANA WAMEBAKI NJIA PANDA KAZI HAKUNA

 
KILA MTU ANAYO HAKI YA KUSHIRIKI KIKAMILIFU KATIKA KULIJENGA TAIFA LETU LAKINI  KUNA HAJA YA KUWEZESHWA KITAALUMA NA NAMNA YA KUTUMIA NGUVU ZAO  ILI KUA NA MAJUKUMU SAHIHI YA KUFANYA

Monday, October 8, 2012

MSINGI WA ELIMU KATIKA KIJIJI CHETU

Bado uhaba wa madawati ni tatizzo kubwa sana ambao unapelekea kukatika tamaa kwa wanafunzi kujua umuhimu wa Elimu na Thamani yake hii inapelekewa kwa kutokuwepo kwa washajiishaji (facilitators)  wenye uwezo katika kusaidia kuondoa hii hali mbovu inayo kumba kizazi hichi kimpya.
 
Ufundishaji duni sana mtoa taaluma anaongea bila mwanafunzi kua na note book, si kweli kama kila kitu kinaingia kichwani na kukaa hii hali inahitaji ushauri na ufatiliaji wa kutosha kuokoa wimbi la wanafunzi wanao feli kwa asilimia kubwa kila mwaka.
Miongoni mwa mambo ya kusikitisha sana ni hili jengo ambalo tulilianzasha kwa nguvu za wazee na wanafunzi tokea 2006 kwa ajili ya kutanua wingi wa madarasa na kusitia hapa hadi leo  bila kujitokeza mfadhili binafsi shirika wala mwanasiasa kati ya tulio wachagua katika kuliendeleza hili na kulimaliza kwa faida ya umma, tunaomba msaada katika kufanikisha hili naamini litakua

JUHUDI ZA KIZALENDO KATIKA KUSUKUMA GURUDUMU LA MAENDELEO KATIKA KIJIJI CHA GANDO WETE PEMBA

  Malighafi kama mdalasini unaweza kusaidia kupungunza umasikini katika kijiji chetu cha Gando na ile dhana ya vijana walio wengi kutegemea tu ajira itapungua siku hadi siku, hivo basi tunawaomba wadau kutoka sehemu mbali mbali kusaidia ushauri na uwezo wa kuwawezesha wakaazi wa mji huu Wa Gando Wete Pemba kuweza ku export mali ghafi zao ili kupambana na janga la umaskini kwa wakaazi.
Huduma ya mawasiliano ni nyenzo moja wapo ya muhimu sana katika kurahisisha njia za maendeleo katika kijiji cha Gando Wete pemba, ukosefu wa mawasiliano ni moja ya kizingiti kikubwa kilichokuwepo dhidi ya mwanga wa maendeleo katika Mji wa Kijiji cha gando, tunashkuru juhudi za kujengwa kwa nyenzo hii ya mawasiliano, tuna ahidi kukanyaga ngazi hii kwa njia zilizo sahihi ili kuleta muamko wa maendeleo katika kijijji hichi kilicho jaa malighafi kama Mwani, mdalasini,asali,pilipili manga,karafuu, bizari,iliki,Mihogo, udongo wenye Rutuba kwa kuzalisha mazao tofauti tofauti, na uwepesishaji wa kufikisha teknologia ya masomo pia kwa kuanzishwa kwa madarasa ya komputa na intaneti.

MWANGA WA MIUNDO MBINU GANDO





Barabara pia ilikua ni moja ya kikwanzo cha maendeleo ya Kijiji cha Gando,hatuna budi kushukuru serikali katika kuleta bara bara japo kua ipo njiani katika kumaliziwa ila hii ni kama taraja la maendeleo, ipo haja sasa ya kutumia Daraja hili la maendeleo ili kupiga hatua za kimandeleo siku hasi siku, tunaihakikishia serikali ya mapinduzi ya zanzibar kua tutatumia miundo mbinu hii mimpya katika nji sahihi kukuza usafirishaji wa mazao kwenda mjini na kutanua wigo wa biashara ya mazao ya ndizi na mengi mengineo.